Khao Sok Thailand, July 2011

Our Tree House

 

Tulitumia usafiri wa barabarani kufika hapa Khao Sok tukitokea Krabi, ilituchukua muda wa masaa 2 na nusu hivi. Tulifikia Baan Khao Sok Resort ambapo tuliamua kuwa na adventure kidogo na kufikia kwenye Tree House kama inavyoonekana kwenye picha. Hii ilikua special kwa Amani na Malaika maana wanapenda sana tree houses. Tulivyofika furaha iliyokuwa usoni mwao ili kuwa na dhamani kubwa. Walianza kuzunguka na kutupa story nyingi tu kuhusu Tree Houses ilikua kichekesho kweli nadhani shule zikifunguliwa itakuwa ndio habari mpya kwa rafiki zao.

Tulikaa hapa kwa siku 3 ila kwa bahati mbaya siku zetu zote tukiwa hapa kulikua na mvua za manyunyu ambazo zinakatika na kuanza. Tulisikitika sana maana plan zetu ilibidi zibadilike tulikua na mpango wa kwenda lake tour ambapo ni lake nzuri sana pamoja na jungle Elephant ride. Ila tuliweza kufanya River Tubing kwenye Sok River ambayo ilikua much fun. Kwa ujumla ilikua real adventure baada ya kulala kwenye Tree House for 3 days tulikumbuka real house maana hapa ilikua ni unyevu unyevu kwenda mbele kutokana na joto lililokua kali na mvua zisizoisha feni haikusaidia sana. Ila kwa upande mwingine tulikua happy kuona watoto wamefurahia sana maana sababu haswa ya kuja hapa ilikua ni kwa ajili yao. Hata baada ya holiday kuisha bado wanaendelea kuzungumzia hii experience. Kwa ujumla ni sehemu nzuri hasa kwa watoto, ila nadhani muda mzuri wa kwenda ni kipindi ambacho si cha mvua hahahaaaa…

Krabi Thailand, July 2011

Amani & Malaika at Phra Nang Beach

 

Ilikua furaha kwetu kurudi tena Krabi and enjoy one of the best beach in the world Phra Nang. Kama kawaida tulifikia Sunrise Beach Resort  tumekua tunafikia hapa since 2003. Uzuri wa Railay kumetulia sana hakuna mambo ya haraka haraka hapa just relax and enjoy if you want to go for a swim, spa or just have a lazy day yote poa tu. Jioni mambo huwa yanachangamka sana hasa Railay beach, I like to sit kwenye mkeka and have a drink huku uki enjoy sunset. That’s way I like it, cheers!!!

Pompeii Naples Italy

Over 2000 years old wall painting. Pompeii City, 2003

 

Tulikuja mji huu special kwa ajili ya kutembelea mji wa Pompeiiambao ulifunikwa na volcano miaka ya 79AD. Ilikua furaha kubwa kwangu kuweza kupata chance ya kutembea kwenye street ambazo watu wa miaka mingi sana walikua wakitumia. Pompeii’s ruins, a jump back to the Roman era in a town destroyed by the Vesuvio eruption in the 79 ad and preserve in a status unique in its kind. 

Tulifika Naples by Train tukitokea Venice tulikaa hapa siku 2. Mjini Naples sikukupenda sana ulikua uko just okey sidhani kama ningependa kurudi tena ila kitu ambacho nilifurahi sana ni kutembelea huu mji wa Pompeii.

Historia ya mji huu inasikitisha sana hasa ukipata nafasi ya kuangalia masalio ya watu na wanyama ambao wamekauka kabisa na moto wa volcano. Inasemekana hakukuwa na taarifa yoyote walichoona ni mwanga kama vile wa jua kumbe ulikua moto mkali sana.

Walivyoufukua mji huu walikuta kila kitu kipo kama kilivyokua kabla ya Volcano ambapo maisha yalikua yanaendelea kama kawaida waliokutwa wakitembea, kulala hata wale waliokua shughulini walikutwa wamekauka hivyo hivyo. Ikanifanya nikumbuke mambo ya biblia kuwa siku ya mwisho hata taarifa haitakuwepo utakapo kuwa ni huko huko. Masalio mengi ya vitu vilivyokutwa kwenye mji huu yameifadhiwa kwenye Museum ya Naples. Kwa upande wangu ilikua funzo kubwa maana kabla ya hapo nilikua sijui kama kitu kama hiki kipo.

@Phoenix Arizona, Utah & Las Vegas, USA. July 2004

 

Stratophere Top of the World Restaurant, Las Vegas

 

Hii ilikua part ya honeymoon yetu. Nachopenda kuhusu hii safari ni kwamba tulidrive all the way to Las Vegas, tulitumia muda wa wiki moja kufika Las Vegas kwa sababu tuliamua kusimama na kulala sehemu mbali mbali on the way.  Pia tulitembelea Meteor Crater pamoja na Grand Canyon ambapo tulilala usiku mmoja. Kwa kusema ukweli safari hii ni moja ya safari ambazo nilizipenda sana mpaka leo imeshapita miaka karibu saba bado naikumbuka kama jana vile, ningependa tena kufanya safari kama hii sehemu nyingine duniani. Hii ilituwezesha kutembelea na kuona maisha ya real Amarican people maana tulikua tunasimama kwenye small town na kulala kwenye small motels.

Wakati tukiwa njiani tulisimama kwenye mji mmoja kuweka mafuta pamoja na kununua drinks. Kwa nini nimekumbuka huu mji ni kwamba ulikua wa kushangaza sana ulikua tofauti sana na miji yote ambayo tumepita, this small town watu wake walikua wako very strange yaani jinsi wanavyovaa ni kama watu wa miaka mingi sana nguo ndefu na ambazo zina staili moja pia wanafuga nywele ndefu kwa wanawake na kufunga kama mabutu mawili au moja. Wanawake wote walivaa staili zinazofanana pia wanaume. Gari letu lilivyokaribia tu kwenye mji huu tuliona watu wanatuchungulia toka majumbani tulivyofika Petrol Station mambo yalikua yale yale. Tukadhani labda upande huu ni ule upande wanaoishi wale wabaguzi wa rangi ukilinganisha mimi ni African tukaona bora mimi nibaki kwenye gari Mr. yeye aingie dukani kwa ajili ya kulipia mafuta na kununua drink.  Aliporudi hata yeye alishangaa sana akasema kwa kweli mji huu uko tofauti bora tundoke mara moja hatukuweza jua kisa na mkasa wa huu mji.

Baada ya mwaka mmoja kupita siku moja naangalia Oprah Winfrey Show then hapo ndipo nilipata jibu. Kumbe mji unaitwa Colorado City ambao uko Arizona, watu wanaoishi hapa wanadini yao ya tofauti inayoamini maisha ya wake wengi pia ni ruska kwa wasichana wadogo kulewa na watu wazima ambao wamewazidi miaka mingi sana. Kitu cha kushangaza ni kwamba watu wengi hawakuwa wanajua kitu kama hiki kiko kwenye nchi iliyoendelea kama America. Wamarekani wenyewe walishangaa na kusikitishwa kuwa kitu kama hiki kipo na kinaendelea nchini kwao. Pia tukajifunza kuwa kuna mengi ambayo yanaendelea kwenye mji huu ambao kwa ujumla ni vya kushangaza pia hawataki wageni kwenye mji wao ndio sababu kubwa ya wao kutuchungulia na kukimbilia ndani. Baada ya kumaliza kuangalia na kuelewa kwa undani nilibaki mdogo wazi na kusema wow!

Baada ya kutoka Colorado City Arizona tuliendelea na safari yetu kama kawaida. Mji mwingine ambao ulinifurahisha sana ni small town call Zion. Iko katikati ya desert ambao umezungukwa na milima mikavu katikati yake ndio kuna huo mji. Tulilala Zion Park Lodge  na kupata nafasi ya kuzungukia mji kidogo nilipapenda kwa kweli ni pazuri sana.

Tulipoanza kuingia Las Vegas mambo yakaanza kubadilika ghafla mambo yakawa ni kufurahisha tu. Tulivyofika tu Stratophere Hotel nilibaki mdogo wazi kama vile nilikua naangalia movie kumbe si movie ni hali halisi hiyo. Tuliposimamisha gari tu wafanyakazi wakaja kwa kasi na kutufungualia milango ya gari huku wengine wakitoa mizigo kwenye gari na kutuomba ufungua wa gari kabla hata sijamaliza kushangaa naona gari letu hilo linaondoka na kwenda sijui wapi yaani lilipotea machoni mwetu ghafla ndio nikakumbuka zile movie nilizokua naona zamani kuwa watu wachukuliwa magari kwenda kupaki mmh! eti leo hii ni mimi nilibaki kutabasabu kabla hayo hayajaisha Mr. ananishika ananishika mkono na tunaelekea hotelini wow! kuelekea reception unahitaji kupitia Casino baadae nagundua kuwa ndio staili ya Las Vegas hiyo karibu hotel zote ziko hivyo.

Tulivyocheck in ikabidi tuzunguke zunguke hotelini hii ni Vegas uwezi kukaa sehemu moja au kulala kila sehemu ni fun tu. Baada ya kuzunguka tukaamua kwenda Casino na nikaamua kucheza Slot Machine ambapo nilikua na kidola changu 20 uwezi amini muda mfupi baadae najikuta nina 200 wacha ninogewe na kuendelea kucheza big mistake baada ya muda kidogo najikuta nimeliwa pesa zote nina ziro mkononi nilichukia huyo, hapo hapo hubby yeye kashinda $120 si nisianze kubembeleza angalau anipe $10 nikiwa na imani kuwa nikicheza nitashinda tena angalau kurudisha pesa zangu. Alichofanya alicheka maana yeye kacheza mara moja kashinda na kaacha kucheza si asinikatalie nilichukia sana nilimnunia karibu siku nzima hata sikuweza kwenda kwenye Stratophere Rides ambapo tulikua na mpango wa kwenda kisa nimeliwa kwenye kamali lol sasa nikikumbuka naishia kucheka si aibu ilioje. Ila ukweli ni kwamba mpaka leo nataka siku nikienda tena Vegas lazima nicheze nilirudisha $200 zangu hahahaaa…

Uzuri sikuacha mambo ya kamali yaniharibie honeymoon na mwisho wake tuliishia kuipenda Las Vegas kupita kiasi, tuliweza tembelea sehemu mbali mbali na kuweza kuenjoy fun za Vegas. Kama kawaida yangu siwezi kwenda sehemu bila kuwa na food favourite, nilipenda sana Strawberry pancakes from  I-Hope, sikuwa peke yangu inaonyesha ni sehemu mashuhuri sana kwa pancakes maana foleni ya kuingia si mchezo ila ukishaingia tu utajua ni kwanini.

Tulikaa Vegas kama siku nne, one night tuliweza kwenda romantic dinner at Stratophere Restaurant Top of the World, ilikua fun maana ukikaa huko juu unaona kama vile jengo linazunguka wacha tubishane na hubby mi nikisema kuwa madirisha yanazunguka yeye anasema hapana ni sisi tunazunguka mpaka tulipomuuliza waiter na kutuambia kuwa ni sisi tunazunguka mh! nikaona hii kali nikaona makubwa ya ulimwengu kwa ujumla tulienjoy sana. Pia tulitembelea Star Trek, hoteli mbali mbali, restaurant na bar tofauti na kila moja ina mvuto wake ni kweli mambo ya Vegas yaache Vegas kwa kweli. Muda wetu wa kukaa hapa ulionekana mdogo sana siku nne hazikutosha kwa kweli lazima turudi tena.

 

@Banyan Tree Hotel Bangkok, Thailand. July 2010

The roof top restaurant, Banyan Tree Hotel Bangkok.

 

Safari hii tulikaa Banyan Tree Hotel Bangkok  baada ya kucheck in tulielekea kwenye room yetu OMG room yetu ilikua wow! Tulichukua Club Suite ambayo ilikua ni breath taking. Baada ya kupumzika kidogo nilimuachia hubby watoto and mum alielekea shopping maana Bangkok na shopping ndio kwenyewe. Usiku hubby treated me a dinner at the roof top restaurant ambayo ilikua amazing and the food was delicous bila kusahau the view is to die for. Kids tuliwaacha na babysitter ambapo Hubby alikua amesha arrange, haya ndio mambo ya Thailand bwana :))))))

The Family Holiday in Koh Ngai, Thailand. 2010

Thanya beach resort

 

Another beautiful Island, was a low season so we had all beach for ourself and that we call fun. We stayed at Koh Ngai Thanya Resort kwenye kisiwa kuna only 5 hotel maana ni kisiwa kidogo tu. Nimeondoka na kumbukumbu ya aina yake toka kisiwani  hapa wacha nidondoke toka kwenye boat siku yetu ya kwanza tu tulivyofika. Bahari kidogo ilikua haijatulia mrembo mimi naanza telemka toka kwenye boat somehow mahesabu yangu yakakataa kutokana na boat kucheza cheza nilichojistukia niko chini mzima mzima na vitu vyangu vyote ndani ya maji kwa kweli ilichekesha sana ila nilichukia kweli pale nilipoona watu wote wanacheka. Maskini simu yangu mpya wacha ilowe na maji ya chumvi ndio ikawa mwisho wake but anyway sikutaka holiday yangu iende vibaya muda mchache ikabidi nichangamke na kuanza kuenjoy and that’s way I like it. Cheers!!!!!

Family Holiday in Khao Kheeo, Thailand. 2010

Flight of the gibbon

 

What an adventure!  Baada ya kuenjoy Pattaya tukaenda Khao Kheeo kupata adventure ya Flight of the Gibbon ni sehemu maalum imetengwa kwa ajili ya national park. Tulifikia Estete ni Tents hotel ina mandhari ya kuvutia sana. Pia nilifurahishwa sana na design ya bathroom zake ambazo zilikua zina usafi wa hali ya juu. Kipindi hiki kilikua ni cha mvua kidogo ambapo kwa upande wangu nilifurahia sana kulala kwenye tents huku mvua inanyesha ilinikumbusha mbali sana enzi hizo nilipokua nafanya kazi Red Cross Kasulu Kigoma Tanzania.

Was nice kuona upande mwingine wa Thailand ambapo huku ni mainland. Na kupata adventure ya kutembelea Zoo mida ya usiku ambapo tuliweza kumsogelea Tiger kwa karibu zaidi and of course without forget Flight of the Gibbon oh dear another new adventure in my life, that’s way I like it. Cheers!!!!

Family Holiday Krabi, Thailand. 2010

At Sunrise resort Krabi with my kids

 

Siamini mara ya kwanza nilikuaja hapa miaka saba iliyopita, hii ni mara yangu ya nne. Kitu cha kuchekesha na kizuri ni kwamba kila tukirudi wanatupa the same room ambayo tulikaa 2003 how sweet. Sunrise Resort and Railay never disappointed us and again we had an awasome time. No adventure this time just relax and enjoy until next time cheers!!!!

Family Holiday Krabi, Thailand. 2009

My baby Malaika at Railay beach

 

We love Railay Krabi, tunazidi kurudi hapa karibu kila mwaka, mambo yanabadilika kwa kasi sana. Maendeleo yanaongezeka mara ya kwanza tulipokuja 2003 kulikua na hoteli chache sana, sasa hivi zimeongezeka maradufu na kufanya kuwepo na choice nyingi ya wapi upate lunch au dinner.

Kitu ambacho bado hakijabadilika ni ukarimu wa watu  nadhani ndio sababu kubwa ambayo inatufanya tuendelee kurudi. Ni sehemu ya kila mtu uwe single, couple au ukiwa na watoto kila mtu atafurahia holiday yake.Sisi bado tunafikia the same hotel kila mara tukiwa Railay Krabi Sunrise Hotel kwa kweli hatuna cha kucomplain kabisa kuhusu hotel hii. Huduma zao ni nzuri sana na wafanyakazi wake ni wakarimu kweli pia bei yao ni ya kuridhisha.

 

 

The Family Krabi, Thailand. 2007

Amani with his brother & sisters

 

This year sikuweza kwenda holiday nilikua niko hoi na ujauzito wa Malaika. Amani and daddy walienda peke yao bila mimi. Huko Thailand walijumuika na our family iliyokua imetokea Australia. My Amani alikua ana mwaka na miezi mitano tu, ila kwa sababu ameshazoea kusafiri hakusumbua kabisa.

Safiri na Zawadi