Category Archives: Tanzania

Dar es Salaam, 2009

At Giraffe Hotel, Mange’s kitchen party

 

Kwa kusema ukweli pamoja na kusafiri nchi mbali mbali duniani siku ambayo najijua nakwenda Dar es Salaam huwa nakuwa na furaha tele maana kuna kitu ambacho huwa najisikia ambacho si cha kawaida ni furaha ilioje pale napoanza kutua kwenye kiwanja cha ndege cha Mwalimu Julius Nyerere huwa napata raha ya ajabu kuwa I’m home now. Kweli naamini usemi usemao nenda West or East Nyumbani ni Nyumbani.

 

Dar es Salaam, 2008 & 2009

Kempinski Hotel

 

Holiday ya kipindi hiki pekee ndio nilipata nafasi ya kukaa kwa muda mrefu nyumbani karibu miezi miwili hivi. Nakumbuka tangu niondoke Dar mwanzo wa mwaka 2002 sijawahi kurudi nyumbani na kukaa zaidi ya wiki 2, kipindi hiki kilikua so special kwangu niliweza fanya mambo mengi ambayo niko proud nayo. Pia niliweza kuwaleta Amani na Malaika kuja kuwatembelea ndugu zao wa huku na familia yangu kupata nafasi ya kuwaona watoto wao. Kitu kingine cha kupendeza ni dada zake Amani & Malaika walipata nafasi ya kuja tembelea Tanzania kwa mara ya kwanza wakitokea Australia. Kila mtu alikua happy kwa kweli….