Sydney Australia, 2004

Nikiwa Old Sydney Holiday Inn Hotel ambapo tulifikia.

 

Nilijikuta nime fall in love kwenye jiji mara tu nilipotua hapa, kimoyo moyo nikaanza plan ya my wedding here. Yap, this year ndoto yangu ikatimia atimaye 1st July 2004 kwenye very old church karibu kabisa na Sydney Harbor ndipo nilipofungia ndoa. Ilikua ni furaha tele hasa pale rafiki yangu mpendwa Stella alipokuja kwa ajili ya harusi akitokea Nairobi  pia baba ambaye alifika siku hiyo hiyo asubuhi akitokea kijijini Burere wilayani Rorya Musoma pamoja kuwa alikua amechoka sana baada ya kuwa angani zaidi ya masaa 24  ila alikua na furaha tele  pale aliponisindikiza na kunikabidhi. Ninafuraha sana kuona ndoto yangu ilikua kweli na kufanikisha kufunga ndoa kwenye jiji hili.

Mipango ya harusi haikuwa rahisi sana kutokana na kuishi sehemu tofauti na mji huu ila tulifanikiwa kumpata wedding planner ambaye alitufanikishia kila kitu na mambo yote ya harusi yalienda safi kabisa. Ila kitu cha kuchekesha ni kwamba mimi ndio kidogo nichemshe na kuchelewa kwenye wedding kisa eti nilikua natafuta sehemu ya kutengeneza kucha kwa style nayotaka. Tukaingia mitaani na rafiki yangu Stella wote tukiwa wageni na sehemu hii tulitafuta mpaka tukapata sehemu na kufanikiwa kutengeneza hizo kucha sasa kasheshe ilikua kurudi hotelini. Wakati tunaenda tulikua tuko busy bila kujali kuangalia tunakokwenda kumbe tulienda mbali sana wacha tupotee kichekesho kweli tukikumbuka. Ila baadae ilibidi tuchukue taxi kama nakumbuka vizuri ya kutufikisha hotelini ambapo nakuta mtu wa make up alishafika siku nyingi na hakuna time ya kufanya hivyo tena, la sivyo tutachelewa kabisa kanisani lol! Ikabidi nioge haraka haraka na kuvaa my dress na kupakwa vitu vidogo tu na kukimbilia kwenye gari na safari ya harusini ilianza yaani ilikua mchaka mchaka kweli, ila nashukuru mungu siku ilienda vizuri na kufanikisha harusi yangu. Kweli hatuachagi asili ya kuchelewa :))))

Tulikua na siku mbili hivi kabla hatujaanza safari yetu ya kuelekea kwenye honeymoon na kutumia muda huo kumtembeza baba around. Kitu kikubwa baba alikua anataka kufanya kabla ajaondoka ni kuwaona Kangaroo hivyo ikabidi tumpeleke Tarongo Park Zoo ambapo aliweza kuwaona na hata kuwashika hao Kangaroo alifurahi sana. Pia tulimpeleka Sydney Tower ambapo aliweza kuona Australia kwenye one room, ndani ya chumba kuna screen kubwa ya tv ambayo inaonyesha helicopter inayozunguka sehemu mbali mbali za utalii wa Australia. Tukiwa tumekaa kwenye viti ambavyo viko kama vya kwenye ndege huku head phone zikiwa masikioni kwetu kwa ajili ya kusikiliza. Wakati hiyo helicopter inakata kona au inachuka kidogo viti vyetu navyo vinafata basi utafikiri nasi tupo pamoja tunaizunguka nchi. Baada ya kumaliza na kutoka baba ndio akatutolea kali tulicheka sana anasema yaani kwa muda mfupi huu tumeweza kuzungukia Australia yote na kurudi kweli hawa wenzetu wametupita mbali sana, alifikiria kuwa katika safari hii nasi tulikua pamoja kwenye hii helicopter, mbavu zetu zilitaka kupasuka kwa kucheka ndio tulimuelewesha nae wacha acheke sana na kuamini kuwa hawa wenzetu ni hatari. Mpaka leo tukimkumbusha huwa anacheka sana

Niliahidi siku nyingi kuwa siku moja nikifanikiwa kwenda kwenye nchi za wenzetu lazima nimpeleke baba nae akapaone hii ilikua ni nafasi nzuri sana ya kumuonyesha dunia ya kwanza wanavyoishi. Baba alifurahi sana tena sana alikua anashangaa kila kitu alivyofika tu toka Airport anauliza  mbona hakuna watu barabarani, kesho yake asubuhi alishangaa sana kuona watu wengi kweli wakivuka barabara wakielekea makazini hapo akasema ok kumbe kuna watu barabarani yaani alikua anatufanya tucheke kila mara hiyo ilikua ni furaha yangu kubwa sana. Alifurahia kila kitu kuanzia usafi wa mji kila akitembea hakuona hata karatasi au vumbi maana Sydney ni moja ya mji msafi duniani ni kusafi sana.

Kwa upande wangu ulikua mwaka wa furaha sana niliweza kufunga ndoa kwenye jiji la my dream, pia kumuona baba yangu akiwa na furaha baada ya kuona nchi za wenzetu wa dunia ya kwanza walivyoendelea, kwangu mimi hiyo ni furaha kubwa sana.

 

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *