Nyoka huyu alikuja msalimia mume wangu alipokua kijijini 2008. Alikua anadonoa donoa kiatu cha Mr. fikiria kama angekuwa hana viatu mbona ingekuwa balaa
Tulijenga kwa muda wa masaa 5 na nusu tu
Kaburi la mdogo wangu Michael
Ujenzi wa kaburi ukiendelea
Barabara ya kijiji
Burere village
Harakati za kukausha samaki kijijini
Sehemu wanayokaushia samaki
Hello Tina
Dala dala boat za huko
Pembeni ya ziwa
Tina kwa raha zake
Wavuvi wakiwa kazini
Tina huyo kwa raha zake kijijini
Flora akiwa kijijini
Kijijini Burere
Love this pic, kijijini Burere
Tina choka kabisa
Mawe haya yanapatikana tu ukanda wa ziwa Victoria
Kijijini Burere
Around kijiji
Around kijiji
Flora kwa raha zake
Tina akiwa Lake Victoria
Look! I'm flying
View ya namna hii inapatikana tu Burere
Wewee...baby sis Tina
Flora kijijini Burere
Jamani mnaona hiyo view? Flora kwa raha zake
Burere
Tina kijijini Burere
Tina akiwa ziwani. Ni mara yake ya kwanza kukanyaga maji ya Lake Victoria
Flora akifurahi na watoto
Garden ya baba kijijini yuko karibu sana na ziwa
Kijijini Burere
Super model toka Burere hahaaa..Flora
Mbona kijiji kilikoma hahahaa...Flora
Flora akifurahia view ya lake
My baby sis Tina
Tina akienjoy upepo wenye afya kijijini
Miguu ya warembo Tina na Flora kijijini, si vumbi hilo
Kaburi la mdogo wangu Michael ambalo tumeenda jenga
Kijijini Burere
Miguu ya masista du kijijini, mbona watanimaliza lol! Flora na Tina
Mrembo Flora kijijini, Aug. 2011
Mrembo Tina akiwa kijijini Burere, Aug. 2011
Mvuvi wa samaki kijijini Burere, jamani sijui huyu Sangara au Sato
Wavuvi wa samaki huko kijijini
Rorya, mdogo wangu kutoka kwa mama mwingine huko kijijini
Watoto kijijini Burere
Watoto kijijini waki enjoy soda. Mume wangu alipiga picha hii 2008
The bridge kwenye river Mara, inasemekana mto huu una mambo wengi na hatari sana
Burere village
Sunset ya nguvu kijijini Burere
Sunset kijini Burere
Sunset in Burere Village
Kijijini burere, mume wangu alipokua huko 2008
On the way to Musoma 2003
Kituo cha basi on the way to Musoma 2003
Mume wangu alimfurahia sana huyu mama, on the way to Musoma 2003
Tulipiga picha hii on the way to Musoma 2003
What a beautiful picture, tulipiga picha hii Musoma 2003
The view of Musoma
Niko pembeni ya Lake Victoria, Musoma 2003
Nimefika hapa kwa mara ya kwanza 2000 ambapo niliamua kwenda kuangalia nilikotoka. Baba alirudi kwao the end of 90’s, na kuweka makazi yake. Naambiwa kuwa nilishaletwa hapa nikiwa na miaka miwili. Kwa sasa baba anaishi kijiji cha Burere, wilayani Rorya mkoani Mara. Kijiji kikiwa karibu sana na Kenya yaani wanasema ukiwa hapa unaweza tembea tu kuingia nchi hii ya Kenya, kwa kweli ni mbali sana tena sana. Ukitaka kuja huku inabidi ujipange kisawa sawa. Tangu mwaka 2000 nimefanikiwa kurudi kama mara mbili hivi zaidi. Ila mara zote hizo sijafanikiwa sana kuzunguka kijijini kwa sababu ya kutokua na muda wa kutosha. Nimekua naingia jioni na kuondoka asubuhi, hata ndugu zangu wengine hapo hawanijui kabisa wananisikia tu. Ila nitapanga siku moja niende ili nipeleke watoto wangu wakapaone nina uhakika watapapenda sana kama baba yao alivyopapenda.
Mwaka huu 2003 tulikua tumetokea Mwanza ambapo tulifika kwa njia ya ndege na kuchukua basi ambalo lilitufikisha Musoma. Mume wangu alifurahi sana kuona mazingira ya barabarani na kupata nafasi ya kushangaa shangaa maisha ya maeneo haya.
Kwa kusema ukweli kijiji hiki ni kizuri sana, mume wangu alipofika hapa hiyo 2008 alishangaa sana uzuri wa kijiji hiki hasa view ya lake Victoria inapendeza kweli. Anasema kuwa kuna fresh air ya ajabu huku ambayo ni adimu sana kuipata. Nakubaliana nae hapa kweli si mchezo na uzuri wake ebu jionee mwenyewe jinsi panavyopendeza.
Mume wangu alipata nafasi ya kuzungukia kijiji na kupiga picha nyingi tu maana alikaa siku nne kwa hiyo alikua na muda wa kutosha kuenjoy fresh air. Kitu kingine kilichomfurahisha sana ni pale watoto walivyokua wakimfuata kila sehemu huku wakimuita mzungu, mzungu akikumbuka huwa anacheka sana. Alifurahi sana kwa kipindi chote alichokua hapa ila anasema kulikua hakuna shower eti alikua anatumia kikombe na ndoo kujimwagia maji anasema laiti kungekuwa na shower. Kweli mzungu aachi asili yake ila kila kitu kingine alipenda sana na alifurahi kweli nao wanakijiji walimfurahia sana kupata mgeni kama yeye.
Aug. mwaka huu nikiwa nimeongozana na ndugu zangu tulifika kijijini kwa njia ya gari ambapo tulidrive toka Dar. Uwezi amini kwenda na kurudi tulitumia zaidi ya kilomita 3000, hakika huku kwetu ni mbali haswa. Tulikuja kwa madhumuni ya kujenga kaburi la mdogo wetu Michael tunashukuru tuliweza kufanikisha hii shughuli kwa haraka na kuweza kurudi Mwanza siku hiyo hiyo. Hatukuwa na muda mrefu maana kaka yangu na wadogo zangu walitakiwa kurudi kazini pia mimi nilitakiwa kurudi kwa watoto wangu ambao walikua karibu ya kufungua shule.
Kwa ujumla nchi yetu Tanzania ni nzuri sana, kuna vijiji vingi ambavyo vina uzuri wa hali ya juu kama serikali yetu ingevitengeneza na kuweka mahitaji muhimu kama vile maji safi, hospitali, shule nzuri, umeme na mahitaji mengi muhimu watu wengi wangekuwa na moyo wa kurudi kuishi huko. Kwa mfano kijiji hiki ni kizuri sana kingeweza kuvutia watalii wengi kama kungekuwa na hayo mahitaji nadhani watu wangeweza hata kujenga nyumba za holiday watu wawe wanaenda pumzika huko maana kwa hii view watalii wangekuja tu.
Flora yuko hoi mafua yamekamata haswa na safari ndio kwanza imeanza
Tumefika Dodoma
Dodoma
Baby sis akiwa Calman Cafe, Dodoma
Flora akiwa Calman Cafe Dodoma
Tukianza kuingia Singida
Beautiful sunset ndani ya Singida
Beautiful Sunset, Singida
Singida
Tulisimama hapa kwa ajili ya kujisaidia
Sunset in Singida
Tukianza safari ya kuelekea Shinyanga
Kutoka Singida kuelekea Shinyanga
Hotelini Mwanza
Mwanza
Tulikumbana na huu ukungu wakati tunatoka Mwanza kuelekea Musoma
Ukungu Mwanza ilikua kazi sana kuendesha gari hakuna kuona
Sunrise Mwanza
Beautiful sunrise in Mwanza
Sunrise Mwanza
Mwanza
Uswahilini Mwanza
Tukiwa tunaingia Shinyanga
Njiani tukiingia Shinyanga
Tukielekea Shinyanga
Njiani kuelekea Shinyanga
Shinyanga
Shinyanga
Shinyanga
Shinyanga
Shinyanga
Shinyanga
Tukitokea Shinyanga kuelekea Singida
Njiani tukitokea Shinyanga kuelekea Singida
Nyumba za vijiji Shinyanga
Kuelekea Singida
Wamasai wakiwa wamevalia kuelekea Gulio karibu na Singida
Njiani tulikutana na gulio karibu na Singida
Gulio karibu na Singida
Mapori ya Singida
Njiani tukitokea Singida kuelekea Dodoma
Njiani kuelekea Dodoma
Tukiikaribia milima ya Sekenke, Singida
Tukiivuta milima ya Sekenke
Milima ya Sekenke, Singida
Tukiwa ndani ya milima ya Sekenke
Tukiwa Senkeke
Milima ya Sekenke
Sekenke
Karibu tukimaliza milima ya Sekenke
Kuna kona kali sana
Kuna kona hatari sana
Tumemaliza salama milima hii ya Sekenke
Tunaingia Singida
Singida
Ili ziwa dogo liko Singida
Tumeanza safari ya kuelekea Dodoma
Sunset Singida
Safari ya Dodoma imeanza
Veta Hotel Dodoma
Veta Hotel Dodoma
Veta Hotel Dodoma
Veta Hotel Dodoma
Gari iliyotupeleka na kuturudisha na kumaliza kilomita zaidi ya 3,000
Veta Hotel Dodoma
Hotel tuliyofikia Dodoma
Dodoma
Bungeni Dodoma
Dodoma
Tulikula chakula kitamu sana hapa, Dodoma
Tulikua tunajiuliza ili gari limepambwa kwa ajili gani haswa tulikosa jibu je wewe unaweza tusaidia. Tulikumbana nalo Dodoma
Group nzima ya safari yetu, kutoka kushoto Hassan, Flora, Hamis na Tina. Dodoma
Nikiwa na kaka Hassan na mdogo Tina, Dodoma
With my kaka nadeka. Dodoma
Love u guys, mwaah!
Tumefanana ehe!
Nyumba vijiji Dodoma
Tukielekea Morogoro, Acacia Tree
Acacia Tree
Tumeanza kuona milima ya Morogoro
On the way to Morogoro
Tumeingia Morogoro
Morogoro
Morogoro
Milima ya Uruguru
Milima ya Uruguru, Morogoro
Milima ya Uruguru, Morogoro
Nikiwa mwanza 2003
Mwanza 2003
The view of the lake from Tilapia Hotel Mwanza 2003
The view of the Lake Victoria
The view from Tilapia Hotel, Mwanza
Safari hii ilikua ni mara yangu ya tatu kuja kwenye jiji hili, tofauti ni kwamba safari zote mbili za mwanzo nilikuja kwa njia ya anga na sio barabara. Hii ilikua ni adventure nzuri sana kwangu na wote ambao tulikua kwenye safari hii, tulianzia safari yetu Dar kupitia Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga then Mwanza. Ni safari ndefu sana ambayo ilikua inatupeleka kijiji cha Burere, wilaya ya Rorya huko Musoma. Tulijumlasha kilomita zote na kupata zaidi ya kilomita 3,000 tulitumia kwenda na kurudi Dar. Safari hii ilituchukua siku nne ambapo tuliweza maliza kilomita zote hizo, tunamshukuru mungu tulisafiri salama na kurudi salama na safari ilikua ya mafanikio makubwa ingawa tulichoka sana.
Madhumuni ya safari hii ilikua ni kwenda kujenga kaburi la mdogo wetu ambaye alifariki karibu miaka 10 iliyopita. Safari hii ilitujumuisha watoto wote wa Fatuma yaani marehemu mama akiwepo kaka yetu mkubwa Hassan, mimi, mdogo wangu aliyenifuata Obuya ambaye tulimpitia Mwanza ndipo anapoishi na mdogo wetu wa mwisho Tina. Pia tulikua na ndugu yetu Flora pamoja na Hamis ambaye alitusaidia sana kwenye maswala ya gari pamoja na udereva, ambapo walikua wanasaidiana na Hassan.
Tulianza safari yetu kutokea Dar saa kumi na mbili asubuhi na tuliwasili Moro mida ya saa 3 asubuhi hivi. Ila tulichelewa kutoka Moro kuelekea Dodoma kwa sababu ya tatizo dogo la gari ambapo ilituweka mpaka mchana ndipo tulianza safari yetu ya kuelekea Dodoma. Tuliwasili Dodoma kwenye mida ya saa tisa jioni hivi baada ya kujisaidia na kupata lunch tulianza safari yetu ya kuelekea Singida. Tuliwasili Singida kwenye mida ya saa kumi na mbili jioni hivi hapa hatukukaa kabisa baada ya kucheki gari na kujisaidia tuliendelea na safari yetu ya Shinyanga. Tuliwasili Shinyanga usiku kwenye mida ya saa nne hivi pia hatukupoteza muda baada ya kucheki gari na kujaza mafuta tulianza safari yetu ya Mwanza, tuliingia kwenye jiji hili kwenye mida ya saa saba usiku tukiwa hoi, choka kabisa na kuamua kulala hapa.
Asubuhi ya saa kumi na mbili tulianza safari yetu ya kuelekea Musoma ambapo tulipitiliza moja kwa moja kuelekea kijijini bila kuingia Musoma mjini. Tuliwasili kijijini kwenye mida ya saa sita hivi na kufanya shughuli iliyotupeleka na kumaliza kwenye saa kumi na mbili jioni na kuanza safari yetu ya kurudi Mwanza, tuliingia Mwanza kwenye saa nne usiku hivi baada ya kutafuta msosi na kula maana tulikua na njaa sana toka tule asubuhi ya siku hiyo hatukula chochote tulielekea hotelini na kulala. Kesho yake asubuhi tulianza safari yetu ila kabla ya kutoka mjini gari lilileta matatizo kidogo ikabidi tulipeleke garage, ilituchukua mpaka mida ya mchana hivi kabla ya kuanza safari yetu ya kuelekea Shinyanga.
Tulianza safari yetu ya kuelekea Dar kupitia Shinyanga, Tabora lakini si mjini, Singida, Dodoma, Moro then Dar. Safari hii tuliamua kulala Dodoma ambapo tulifika hapa kwenye saa mbili au tatu usiku hivi. Tulipata nafasi kwenye Veta hotel ambayo kwa ujumla ilikua nzuri. Kesho yake asubuhi tulielekea kwenye makaburi ya Kizota kwenda kutizama kaburi la mama ambapo alizikwa karibu miaka 21 iliyopita. Baada ya hapo tulipata breakfast na kuanza safari yetu ya kuelekea Dar mnamo karibu saa tano hivi.
Tuliwasili Dar kwenye mida ya saa kumi jioni hivi ila kutokana na foleni ilitufanya kuwasili home kwenye saa kumi na moja jioni. Kwa kweli safari hii ilikua ya mafanikio makubwa, ilikua ni adventure nzuri sana ambapo wote tuliokuwa kwenye msafara huu tunakubaliana nalo sote tulifurahi sana. Nina plan ya kurudia tena hii safari in the future ila this time nataka nisiwe na haraka ili nipate muda wa kulala kwenye mikoa yoyote hii ili nipata muda mzuri wa kuitembelea sio kama hii safari ambapo tuliingia na kupita tu. What an adventure, I love it!
Nikiwa Old Sydney Holiday Inn Hotel ambapo tulifikia.
Nikiwa Old Sydney Holiday Inn ambapo tulikua tumefikia. View hapa juu ni amazing!
Nikiwa na rafiki yangu Stella
Tukiwa George Street na rafiki yangu Stella
Tukiwa na rafiki yangu Stella mitaa ya Sydney usiku
Nikiwa na baba Sydney Harbour
Tukiwa Sydney Tower
Nikiwa na rafiki yangu Stella
Siku ya harusi yangu
Siku ya harusi yangu
Nilijikuta nime fall in love kwenye jiji mara tu nilipotua hapa, kimoyo moyo nikaanza plan ya my wedding here. Yap, this year ndoto yangu ikatimia atimaye 1st July 2004 kwenye very old church karibu kabisa na Sydney Harbor ndipo nilipofungia ndoa. Ilikua ni furaha tele hasa pale rafiki yangu mpendwa Stella alipokuja kwa ajili ya harusi akitokea Nairobi pia baba ambaye alifika siku hiyo hiyo asubuhi akitokea kijijini Burere wilayani Rorya Musoma pamoja kuwa alikua amechoka sana baada ya kuwa angani zaidi ya masaa 24 ila alikua na furaha tele pale aliponisindikiza na kunikabidhi. Ninafuraha sana kuona ndoto yangu ilikua kweli na kufanikisha kufunga ndoa kwenye jiji hili.
Mipango ya harusi haikuwa rahisi sana kutokana na kuishi sehemu tofauti na mji huu ila tulifanikiwa kumpata wedding planner ambaye alitufanikishia kila kitu na mambo yote ya harusi yalienda safi kabisa. Ila kitu cha kuchekesha ni kwamba mimi ndio kidogo nichemshe na kuchelewa kwenye wedding kisa eti nilikua natafuta sehemu ya kutengeneza kucha kwa style nayotaka. Tukaingia mitaani na rafiki yangu Stella wote tukiwa wageni na sehemu hii tulitafuta mpaka tukapata sehemu na kufanikiwa kutengeneza hizo kucha sasa kasheshe ilikua kurudi hotelini. Wakati tunaenda tulikua tuko busy bila kujali kuangalia tunakokwenda kumbe tulienda mbali sana wacha tupotee kichekesho kweli tukikumbuka. Ila baadae ilibidi tuchukue taxi kama nakumbuka vizuri ya kutufikisha hotelini ambapo nakuta mtu wa make up alishafika siku nyingi na hakuna time ya kufanya hivyo tena, la sivyo tutachelewa kabisa kanisani lol! Ikabidi nioge haraka haraka na kuvaa my dress na kupakwa vitu vidogo tu na kukimbilia kwenye gari na safari ya harusini ilianza yaani ilikua mchaka mchaka kweli, ila nashukuru mungu siku ilienda vizuri na kufanikisha harusi yangu. Kweli hatuachagi asili ya kuchelewa :))))
Tulikua na siku mbili hivi kabla hatujaanza safari yetu ya kuelekea kwenye honeymoon na kutumia muda huo kumtembeza baba around. Kitu kikubwa baba alikua anataka kufanya kabla ajaondoka ni kuwaona Kangaroo hivyo ikabidi tumpeleke Tarongo Park Zoo ambapo aliweza kuwaona na hata kuwashika hao Kangaroo alifurahi sana. Pia tulimpeleka Sydney Tower ambapo aliweza kuona Australia kwenye one room, ndani ya chumba kuna screen kubwa ya tv ambayo inaonyesha helicopter inayozunguka sehemu mbali mbali za utalii wa Australia. Tukiwa tumekaa kwenye viti ambavyo viko kama vya kwenye ndege huku head phone zikiwa masikioni kwetu kwa ajili ya kusikiliza. Wakati hiyo helicopter inakata kona au inachuka kidogo viti vyetu navyo vinafata basi utafikiri nasi tupo pamoja tunaizunguka nchi. Baada ya kumaliza na kutoka baba ndio akatutolea kali tulicheka sana anasema yaani kwa muda mfupi huu tumeweza kuzungukia Australia yote na kurudi kweli hawa wenzetu wametupita mbali sana, alifikiria kuwa katika safari hii nasi tulikua pamoja kwenye hii helicopter, mbavu zetu zilitaka kupasuka kwa kucheka ndio tulimuelewesha nae wacha acheke sana na kuamini kuwa hawa wenzetu ni hatari. Mpaka leo tukimkumbusha huwa anacheka sana
Niliahidi siku nyingi kuwa siku moja nikifanikiwa kwenda kwenye nchi za wenzetu lazima nimpeleke baba nae akapaone hii ilikua ni nafasi nzuri sana ya kumuonyesha dunia ya kwanza wanavyoishi. Baba alifurahi sana tena sana alikua anashangaa kila kitu alivyofika tu toka Airport anauliza mbona hakuna watu barabarani, kesho yake asubuhi alishangaa sana kuona watu wengi kweli wakivuka barabara wakielekea makazini hapo akasema ok kumbe kuna watu barabarani yaani alikua anatufanya tucheke kila mara hiyo ilikua ni furaha yangu kubwa sana. Alifurahia kila kitu kuanzia usafi wa mji kila akitembea hakuona hata karatasi au vumbi maana Sydney ni moja ya mji msafi duniani ni kusafi sana.
Kwa upande wangu ulikua mwaka wa furaha sana niliweza kufunga ndoa kwenye jiji la my dream, pia kumuona baba yangu akiwa na furaha baada ya kuona nchi za wenzetu wa dunia ya kwanza walivyoendelea, kwangu mimi hiyo ni furaha kubwa sana.
With my brother Hassan and baby sis Tina at the Airport. Love this guys kupindukia
With my brother Hassan, nasema asante sana kaka.
With my brother Hassan
With my brother Hassan, mi penda sana weye
The family
With my brother Hassan and baby sis Tina at the Airport. Love this guys kupindukia
At the Airport with my brother Hassan & baby sis Tina, love u sana sana guys
My wifi Mariam, love u Mamu sana tu.
Mambo ya siku ya Eid hayo, too bad nilikua naondoka baada ya masaa machache hapo
With my old friend Blandina tangu tukiwa 11yrs old
Southern beach Kigamboni
Kipepeo beach Kigamboni
With my old friend Sarah since the 90's
Flora
Masaki Sea Cliff
Masaki Sea Cliff
Sea Cliff
Happy Flora
Flora at Sea Cliff Hotel
Flora wangu huyo
Sea Cliff Hotel
The view from Sea Cliff Hotel
Aawww..Mama Doris what a strong woman, tunakupenda sana.
With Alice, Agnes & Emmy
With Alice, Agnes & Emmy
Mdogo wangu huyo pendeza weye
Baby sis Tina
Watengenezaji wa BBQ
Mambo ya Kiti Moto hayo
Linda's farewell party at Uncle Gondwe & Aunt Sarah place
Mambo ya BBQ
At Linda's farewell party
Uncle Gondwe & Aunt Sarah place
Uncle Gondwe & Aunt Sarah place
Jimmy, Tina & Queen
Warembo wetu
Yummy!
Mambo ya wifi yangu hayo
Muda wa kufuturu huo
Mambo ya kufuturu hayo kwa mamu
Safari hii ilikua ya mafanikio sana ambayo ilinipeleka mpaka kijijini Musoma. Nilikaa Dar kwa kipindi kifupi tu ila nilifurahi sana hasa kwa kupokelewa vizuri na wifi na kaka yangu, asanteni sana guys! Pia kitu kikubwa ambacho kilinifurahisha kuliko ni kuweza kufanikisha kilichonileta na pia kukutana na watoto wate wa Fatuma, I hope mama huko aliko alismile kwa furaha. Ni muda mrefu sana tangu sote tuwe pamoja karibu miaka 15 hivi na kuweza kufanikisha kitu muhimu kwetu sote. Kitu kingine ambacho this time nilienjoy sana ni misosi wifi yangu ni mtaalam kwa mambo haya basi si kupika, wacha tule, I wonder why niliongeza more than 3kg kwa chini ya siku 10 tu. Kwa ujumla this trip ni ya furaha kubwa..
With Amani & Malaika at Life Park ready for adventure
Malaika & Amani at Life Park
With my kids, nyuma yetu ni swing ambayo ilinitoa kichefu chefu siku nzima baada ya kuipanda
Little cow girl
Little cow boy & cow girl
Dada mtu huyo
Happy kid
The little small town
Here she comes
Amani love it
Fun inaendelea
Amani having fun at life park
Malaika having fun at Life Park
Beautiful pool
My family hao wanaenda kwenye pool after lunch
The hotel pool
The view of the pool from restaurant
Beautiful pool
Splash!
Fun fun fun at the pool side
Walifurahi sana
The hotel pool side
Here she is
For sure, he's having fun
My Amani
Here he goes
Here she goes
Here he comes
Here she comes
The kids having fun at the pool
The hotel pool by night
The view of the pool night time
The view of the hotel, night time
Amani at the restaurant
One of the hotel restaurant
One of the hotel restaurant
Inside restaurant
Around the hotel
Around hotel
The hotel
The hotel
Nasi pia tunaelekea huko
Elephant ride adventure
Italian Mall in the middle of the jungle, yaani inashangaza kweli hii mall ni nzuri sana iko the middle of nowhere ila inapendeza sana.
The restaurant in the hotel
The girls at the restaurant
Inside Sports Lounge in the hotel
Tulikwenda Sports Lounge after dinner
Hotel lobby
At the hotel lobby
Malaika at the hotel lobby
Malaika at hotel lobby
The room
The room
Lunch time
What's for lunch? Fried Flowers and Green Papaya Salad
Lunch time yummy! Green Papaya Salad
Green Papaya Salad, one of my favourite
It's lunch time
Waliipenda sana hii pool
Amani loves it
Amani & Malaika having blast
The hotel pool
Amani loves the pool too much
Watch out Amani, splash!
Malaika at the pool
Vintage car around the hotel. Kaka Hassan unaona mambo hayo?
Malaika on Courtesy bus
At the ranch
Heey Yaah!
At the ranch
Little cow boy & cow girl
Now with tractor
Kids having fun
Amani having fun
Wakiangalia usalama tayari kwa adventure ya Flying Fox
Amani alikua anaogopa kweli, thanks to the little boy aliyemshawishi kwa kumwambia kuwa iko awesome is one of the life time adventure, better to try it! The word
Hao wanaenda
I can see them, what an adventure for kids. Waliipenda sana
Hao wanakuja wakiwa kwenye Flying Fox
Wakimalizia their Flying Fox
Hao wamemaliza, Amani loves it mpaka alikwenda kwa mara nyingine
Hubby nae huyo anakuja akiwa kwenye Flying fox
My family baada ya kumaliza their adventure Flying fox
I hate this ride, this swing ilinifanya nijisikie kichefu chefu siku nzima jamani
My Amanji loves cars
And here she comes, splash! My Malaika
And here he comes splash! My Amani
Huku mama kajipumzisha and watching them
Hao wanakatiza
My family swimming
Mrembo wangu kajiamulia kujisomea huku akiwa anasubiri that another sifa ya Malaika
Tukisubiri zamu yetu ya kupanda Elephant
The man alitusaidia kutuongozea Elephant wetu kwenye mto
Pande hii ya Thailand hatujawahi kuufiki hii ilikua ni mara yetu ya kwanza. Tulikuja special kwa ajili ya Greenery Resort ambayo iko famous sana kwa ajili ya watoto na familia nzima kwa ujumla. Kuanzia makaribisho mpaka huduma yote ilikua nzuri sana. Amani & Malaika walifurahia sana hii ilikua special kwa ajili yao. Kitu cha kwanza walichoona tulivyofika tu ilikua ni hotel pool ambayo ilikua amazing. Pia walipata nafasi ya kutembelea The life park ambayo iko chini ya hotel ambayo ina michezo mingi sana ya watoto. Bila kusahau Elephant(Tembo) ride adventure ambayo ilikua awesome.
Hotel ina aina tofauti za room zikianzia za chini kabisa mpaka za juu, sisi tulichukua this time standard room. Muda wetu mwingi tulitumia nje kwenye michezo ya watoto hatukuona haja ya kuchukua room nzuri sana maana hatutaitumia sana zaidi ya kulala tu. Tulikaa hapa for 3 nights watoto walifurahi sana wanasema kuwa ni one of their favourite hotel this summer holiday.
Nilipokutana na rafiki mpya tukiwa maeneo ya Sinza
Maeneo ya Mabibo nimekaa huku jamani
Level 8 Kempinski Hotel
Baby sis Tina at Kempinski Hotel
Dar by night
Posta by night
The view from level 8 Kempinski Hotel
Night out at Kempinski Hotel
The view from Bongoyo Island
At Bongoyo Island beach
At Bongoyo Island beach
Tina & Flora at Bongoyo Island
Beautiful beach, Bongoyo Island
Bongoyo Island, beautifu beach with white sand
Bongoyo Island
At Bongoyo Island
Bongoyo Island
Bongoyo Island, beautiful beach
My baby sis Tina
Boat iliyotufikisha beach
Flora akiwa kwenye boat ndogo inayotufikisha Bongoyo Island kabisa
Baby sis Tina
The Bongoyo Island
The Bongoyo Island
Flora in the boat
Near Yatch Club
The view of Masaki from the boat
With baby sis Tina at Slipway on our way to Bongoyo
Tina & Flora at Slipway on our way to Bongoyo Island
With baby sis Tina at Kempinski Hotel
Kempinski Hotel
Kipepeo Village Beach Kigamboni
Nikiwa Kipepeo Village Kigamboni
Flora at Kipepeo Village Kigamboni
At Kipepeo Village Kigamboni with vijana Deborah, Tina & Flora
At Kipepeo Village Kigamboni
Safari hii niliamua kwenda kupumzika kidogo peke yangu. Nilipata nafasi nzuri ya kukaa na mdogo wangu this time pia nilipata nafasi ya kumpeleka mdogo wangu wa mwisho kwenda kuangalia kaburi la mama huko Dodoma, kitu ambacho najivunia sana maana baada ya kufika na kuliona roho yangu ilisuhuzika mno nadhani huko aliko anasmile.
With Kay & baby sis Tina at Golden Tulip Salsa night
Malaika
Malaika with her cousin Mikiko(Imani)
At Slipway
Malaika with Masai at Kipepeo Beach
Malaika at Kipepeo Beach
Ndani ya kivuko
Watu wakitoka ndani ya kivuko
Kivuko kinachovusha watu kuelekea na kutoka Kigamboni
Kivuko
With Malaika at Marry Brown
Southern Beach Kigamboni
At Slipway
Nikiwa na Malaika Slipway
Malaika & Ryan tukiwa lunch pale Rose Garden
Kigamboni feri
Malaika na Kifaranga
Tembelea ndugu na jamaa, Malaika akifurahia Kifaranga
Southern Beach Kigamboni
Malaika akicheza Kipepeo beach
Malaika wangu akiwa Kipepeo beach
Malaika akifurahia beach Kipepeo
Malaika at Kipepeo beach Kigamboni. Beautiful beach
Malaika at Slipway
At Slipway
At Slipway
Malaika akiwa Slipway
Nilikwenda msalimia rafiki Christina ofisini kwake pale Masaki
Mdogo wangu Tina, Check point posta for lunch
Malaika at Jaki place
Malaika with her bibi mkubwa at Jaki place
With Malaika ndio kwanza tumewasili
With Malaika & Flora, Airport tukiwa ndio tumewasili
Golden Tulip Hotel, Theo akinifundisha kucheza Salsa.
With Kay & mdogo wangu Tina. Salsa night at Golden Tulip Hotel
Bongo by night
With my old friend Mage toka Sec School
Malaika alifurahia sana Tanzania maana this time alikua amekua kidogo anaelewa karibu kila kitu. Neno alilochukua sana ni Jambo, basi yeye kila mtu mweusi anamuita from Jambo maana anamuita mama yake ametokea Jambo eti ndio Tanzania, watoto bwana wanachekesha sana, basi akiitamka hiyo jambo yake sasa inaleta raha kweli.
At Clara & Nicas place. Amani & Malaika with family Adili, Shakwana, Shanira & Asante
With Bella at wedding ceremony
With Farida & Bella
With Bella at Mange's wedding reception Kempinski Hotel
With Farida
With Neema and her sister
With Sumai
With Killy & Aisha
With Jack & Killy
At reception party Kempinski Hotel
With Bride & Groom
Amani & Malaika with dada Flora at Mlimani City Mall
With my kids
With Amani & Malaika at Mlimani City Mall
Kwa kusema ukweli pamoja na kusafiri nchi mbali mbali duniani siku ambayo najijua nakwenda Dar es Salaam huwa nakuwa na furaha tele maana kuna kitu ambacho huwa najisikia ambacho si cha kawaida ni furaha ilioje pale napoanza kutua kwenye kiwanja cha ndege cha Mwalimu Julius Nyerere huwa napata raha ya ajabu kuwa I’m home now. Kweli naamini usemi usemao nenda West or East Nyumbani ni Nyumbani.
At the Mwalimu Julius Nyerere Airport with Billy, baby Malaika, Stella & Bobby
Mambo ya msosi at Obuya's place. Bongo na misosi inanimaliza kabisa
My younger brother Obuya
At Obuya's place
At Obuya place
Baby Sis Tina ujaacha asili yako, msosi kwanza ehe!
With baby Malaika & Amani outside Sea Cliff
With Stella & Marina at Sea Cliff
Stella, baby Malaika, Amani & Bobby at Kenny's house
At Slipway with baby Malaika
Night out with Stella
Night out with Stella
at Slipway with my family
Baby Malaika with aunt Judy on the boat to Bongoyo Island
On the boat to Bongoyo Island, Billy, Amani, Bobby & Hubby
On the boat to Bongoyo Island
Going to Bongoyo Island
With hubby, going out for dinner
With Halima at Leaders Club Miss TZ 2008
Amani & baby Malaika at Kipepeo Village beach
Sameera birthday party at Kipepeo Village, Kigamboni
Malaika with friend
Kenny's place
Kenny, baby Malaika & her friend
Sasha's birthday party. Amani & Sasha
Holiday ya kipindi hiki pekee ndio nilipata nafasi ya kukaa kwa muda mrefu nyumbani karibu miezi miwili hivi. Nakumbuka tangu niondoke Dar mwanzo wa mwaka 2002 sijawahi kurudi nyumbani na kukaa zaidi ya wiki 2, kipindi hiki kilikua so special kwangu niliweza fanya mambo mengi ambayo niko proud nayo. Pia niliweza kuwaleta Amani na Malaika kuja kuwatembelea ndugu zao wa huku na familia yangu kupata nafasi ya kuwaona watoto wao. Kitu kingine cha kupendeza ni dada zake Amani & Malaika walipata nafasi ya kuja tembelea Tanzania kwa mara ya kwanza wakitokea Australia. Kila mtu alikua happy kwa kweli….
Hubby & Malaika in Thai Airways from Phuket to Bangkok
Ciem Paragon Mall
Awww…Lebua, hapa kila kitu 1st class kuanzia unavyoingia mpaka unavyotoka. Tulikaa Lebua State Tower Hotel for 3 days nilitamani zisiishe mapema. Our summer holiday inaendelea tumeingia hapa tukitokea Phuket. Naweza sema I love everything about this hotel, huduma yake ni ya kukata na shoka. Unapoingia tu unasikia harufu ya upendo moja kwa moja kwanza hotel staff anakuja kukupokea kwa upendo wa hali ya juu na kukukaribisha kukaa na huku akiwa na file lako la kucheck inn, ina maana alikua anawasubiri nyinyi specially na akimaliza kupata data zote anawasindikiza kwenye room yenu huku akiwapa maelezo muhimu kuhusu hotel with big smile. Wamefanikiwa kumfanya kila mteja kujisikia ni most important kwao nadhani hii ni huduma ya 1st class kwa kweli. Kwa wale mtakaojikuta Bangkok please jaribu hii hotel nadhani utakubaliana nami. Very happy indeed until next time Labua State Tower Hotel, cheers!!!